Drogba Akatwa Urais wa FIF
KAMATI ya uchaguzi ya shirikisho la soka Ivory Coast (FIF) imemuengua mchezaji wa zamani wa Chelsea na timu ya taifa ya Ivory Coast, Didier Drogba, katika kinyang’anyiro cha kuwania urais wa FIF kwa kudaiwa hati zake hazikukidhi vigezo.
Inadaiwa Drogba alikuwa anaapewa kipaumbele zaidi katika mbio za kuwania Urais wa FIF katika uchaguzi mkuu wa FIF unaotarajiwa kufanyika Septemba 5, 2020.
Kwa kuenguliwa huko, Drogba amepoteza nafasi ya kuwania nafasi ya urais na kuwaacha Sory Diabate na Idriss Diallo katika mbio za kuwani urais huo.