DSJ Wtumia Umafia Kuipiga Global FC
KOCHA wa Global FC, Amran Kaima, amesisitiza kwamba walitumia uungwana kucheza na DSJ FC kuhofia vurugu za mashabiki waliokuwa wanawasubiri kwa hamu. Katika mchezo huo wa kirafiki, Global FC ilipoteza kwa mabao 3-1 kwenye uwanja wa Boom, Ilala.
Akizungumza kwa hisia kali na Spoti Xtra, Kaima maarufu kama Zahera alisema uwanja huo ulikuwa chakavu na mastaa wake hawajazoea kucheza kwenye vumbi ndio maana wakawa muda mwingi wakishangaa na hawakuwa wakiamini wanachokiona.
Comments are closed.