Dstv yaja na chaneli ya maisha magic Bongo, kwa ajili ya Watanzania
Mkurugenzi M-Net Kanda ya Afrika Magharibi, Wangi Mba-Uzoukwu akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kutoka nchi za Afrika waliokusanyika kwenye jukwaa kubwa la kuonesha vitu mbalimbali vinavyoburudisha katika chaneli za DStv na GoTv kupitia MultiChoice hivi karibuni nchini Mauritius.
Mkurugenzi wa M-Net kwa nchi za Afrika Mashariki na SADC, Theo Erasmus akifurahi jambo kwenye mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) kutoka nchi mbalimbali za Afrika.
Mkuu wa chaneli ya Maisha Magic, Margaret Mathore akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani).
Pichani ni waandishi wa habari kutoka nchi mbalimbali za Afrika waliokusanyika kwenye jukwaa hilo lililoandaliwa na MultiChoice Africa hivi karibuni.
Mkurugenzi M-Net Kanda ya Afrika Magharibi, Wangi Mba-Uzoukwu (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Movie Stars wa nchini Nigeria, Rita Dominic na Desmond Elliot mara baada ya mkutano na waandishi wa habari.