The House of Favourite Newspapers

Dube Awatesa Makipa Azam

0

MSHAMBULIAJI wa Azam FC na raia wa Zimbabwe, Prince Dube, amewatesa makipa wa Azam kwenye mazoezi.Mzimbabwe huyo ni kinara wa mabao Ligi Kuu Bara akiwa nayo 12, akifuatiwa na Meddie Kagere mwenye mabao 11.

 

Kwenye mazoezi yao yaliyofanyika juzi katika Uwanja wa Azam Complex, mwalimu George Lwandamina aligawa timu mbili kwenye kikosi chake, Timu Dube Vs Timu Monzinzi, mchezo huo ulimalizika kwa timu Dube kufunga mabao 4-0.

 

Dube aliyefunga mabao matatu na asisti moja ya goli aliyompa Never Tigere, alichezewa rafu nne akacheza moja na kukosa bao moja.

 

Azam wapo nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara wakiwa na pointi 54, baada ya kucheza michezo 28, wakiwa nyuma ya vinara Simba kwa tofauti ya pointi saba huku Wekundu wakiwa wamecheza michezo 25.

STORI: CAREEN OSCAR, Dar es Salaam

Leave A Reply