The House of Favourite Newspapers
gunners X

Dunia Yamlilia Maradona

0

GWIJI  wa zamani wa kandanda, Diego Maradona, amefariki dunia jana akiwa na umri wa miaka 60 kwao Argentina ambapo mapema mwezi huu, Novemba, alifanyiwa upasuaji wa ubongo ambao madaktari walimwambia ulifanikiwa.

 

Baada ya kutangazwa kwa kifo hicho mastaa mbalimbali wamemlilia Maradona kupitia kwenye  kurasa zao kwenye mitandao ya kijamii, na Rais wa Argentina, Alberto Fernández,  ametangaza siku tatu za maombolezo nchini humo.

Lionel Messi

Kwa upande wa Messi ambaye  amekuwa mara kwa mara  akilinganishwa na nyota huyo, alifanya kazi na Maradona wakati anaifundisha timu ya taifa ya Argentina wakat fainali za Kombe Dunia mwaka 2010 zilizofanyika Afrika ya Kusini.  Kupitia mtando wa Instagram, Messi ameandika:

“Waargentina na dunia wanapita kwenye wakati mgumu sana. Diego ametutoka kimwili lakini anaishi ndani ya mioyo yetu, daima nitaendelea kuzienzi  kumbumbuku zako, natanguliza salamu zangu za pole kwa familia na marafiki na wapenzi wote wa  mpira wa miguu”.

Cristiano Ronaldo 

Naye nyota wa timu ya taifa ya Ureno, Ronaldo amesema dunia imepoteza rafiki na mkali wa soka kuwahi kutokea.  “Umeondoka mapema na  pengo lako halizibika kamwe,” ameandika mtandaoni.

Pele

Mchawi wa soka kutoka Brazil, Pele, amesema amepoteza rafiki na lejendi wa soka na anaamini siku moja watacheza tena mpira mbinguni.

FC Barcelona

Klabu ya Barcelona imeandika kwenye mtandao: “Asante kwa kila kitu”.  Maradona aliwahi kukipiga kwenye timu hiyo yenye maskani yake Catalunya.

Gary Lineker

Mmoja ya wachezaji waliokuwepo wakati Maradona anafunga kile kilichokuwa maarufu kwa kujulikana kama “bao la mkono” dhidi ya England ni Gary Lineker ambaye kwa sasa ni mtangazaji katika kituo cha runinga cha Sky Sports.  Naye  amemwelezea  kama mchezaji bora katika kizazi chao wakati wanasakata kabumbu.

SSC Napoli

“Licha ya kupita katika vilabu kadhaa barani Ulaya.  Timu ya Napoli ndipo palikuwa  nyumbani kwake, na amepata mafanikio mengi akiwa hapa,” imeandika klabu hiyo mtandaoni.

Rasmi klabu hiyo imetangaza kuwa wataupa uwanja wao jina la Maradona kwa heshima ya gwiji huyo.  Kwa sasa uwanja huo unaitwa San Paulo Stadium ukiwa ni wa tatu kwa ukubwa nchini humo  baada ya Stadio Olimpico na San Siro.  Una uwezo wa kuchukua watazamaji 55,000.

 

Leave A Reply