Watoto wakijiachia kwenye bembea la kuseleleka
Shoo ya kihistoria itakayofanyika katika siku hii ya Idd Mosi pale watakapovamia jukwaa moja la Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live wakali kibao wanaotikisa kwa michano Bongo wakiongozwa na R.O.M.A Mkatoliki, Darassa, Stamina na Mr Blue na kumaliza ubishi wa nani mkali wa michano.
Watoto pia wamepata burudani kutoka Kundi la Muziki wa Asili la Makhirikhiri kutoka Tanzania, Wakali wa Sarakasi, Wakali Dancers pamoja na mkali wa vichekesho, Bambo atakayehakikisha amevunja mbavu watoto wote, pamoja na michezo ya watoto ya kuogelea kama picha zinavyoonyesha.
Watoto wakiogelea Dar Live
Mtonyo sasa!
Watoto wote kiingilio kitakuwa sawa na bure kwani getini watapita kwa pesa kiduchu sana yaani shilingi 3,000 tu, huku wakubwa nao sawa na bureeeeeee, yaani 7,000 tu getini unaachiwa huru kabisa umshike mkono R.O.M.A, Darassa, Stamina, Mr Blue, Snura au waimbaji wa Zanzibar Stars.
OVER ZE WEEKEND
Watoto full kujiachia.
Watoto wakibembea
Wakishindana kucheza muziki.
PICHA NA DENIS MTIMA/GPL