The House of Favourite Newspapers

EMINA INAVYOONGOZA KUSAMBAZA MADAWA YA USAFI MAJUMBANI

 Afya njema ni utajiri wa kwanza kwa binadamu! Huwezi kushiriki kwenye shughuli zozote za kimaendeleo iwapo afya yako haipo sawa na katika kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. John Pombe Magufuli za kuhakikisha Tanzania inafikia uchumi wa kati na viwanda, kampuni ya Emina imeelekeza nguvu zake kuhakikisha Watanzania wanakuwa na afya bora.

Kampuni ya Emina yenye makao makuu yake Upanga, jirani na Shule ya Olympio jijini Dar es Salaam, ni watengenezaji na wasambazaji wa bidhaa mbalimbali, kubwa ikiwa ni Septol, dawa yenye uwezo mkubwa wa kuua vijidudu vya maradhi kwenye maeneo mbalimbali, kusafishia vidonda, kufanyia usafi mahospitalini, majumbani, vyooni, saluni na sehemu nyingine zinazoweza kuwa mazalia ya bakteria, fangasi na virusi.

Mbali na Septol, bidhaa nyingine zinazozalishwa na kusambazwa na Emina ni dawa ya meno iliyotengenezwa kwa mimea asili, yenye uwezo wa kupambana na maambukizi ya bakteria kinywani, kung’arisha meno na kuzuia meno kuoza.

“Pia tunasambaza bidhaa mbalimbali kwa ajili ya usafi wa nyumbani na maofisini kama glass cleaner ambayo kazi yake ni kusafisha vioo vya madirishani, milangoni, kwenye makabati na kadhalika na kuvifanya vionekane kama vipya, Tile and Ceramic Cleaner maalum kwa ajili ya kusafisha vigae, marumaru, masinki ya kunawia mikono na masinki ya vyoo na kuondoa uchafu sugu,” anasema Zahara Mohamed, mwakilishi wa kampuni hiyo na kuongeza:

“Pure Pine Cleaner ni maalum kwa ajili ya usafi wa hospitalini, mashuleni, nyumba za wageni, majumbani na migahawani na unaweza kuitumia kusafishia tiles, sakafu, jiko, mifereji, masinki, bafu na vyoo. Inao uwezo mkubwa wa kuua vijidudu na kukufanya uwezo kwenye mazingira salama wakati wote.”

“Bidhaa zetu zinapatikana nchi nzima na tunaweza kukuletea mahali ulipo kama unahitaji oda kubwa, unachotakiwa kufanya ni kuwasiliana na wauzaji wetu waliopo jirani na wewe. Kwa jijini dar es Salaam, ofisi zetu zipo Upaanga jijini Dar es Salaam na unaweza kuwasiliana nasi kwa namba 0745 215 253 au 0688 618 139.

“Kwa wale waliopo mikoani, wanaweza kuwasiliana na wauzaji wetu kama ifuatavyo: Mwanza, Mara, Geita na Shinyanga, piga simu namba 0763 699 918, kwa Arusha, Manyara na Simiyu, piga namba 0764 559 026.

“Kwa wateja waliopo Kilimanjaro, Tanga na Kigoma, wawasiliane na wauzaji wetu kwa namba 0784 744 410, wale wa Njombe wapige namba 0759 185 344, Lindi na Mtwara namba 0757 409 134, Dodoma, Singida na Tabora namba ni 0716 664 444 na kwa wale wa Bukoba, Katavi na Rukwa, wapige namba 0752 104 085,” alisema Zahara.

UTACHEKA! Mama Lishe Tandale Waelezea Sababu za Kukimbiwa na Wateja

Comments are closed.