The House of Favourite Newspapers

EPL: Chelsea, Tottenham ngoma suluhu

1

Clinton N’Jie wa Tottenham akikwaana na Cesc Fabregas wa Chelsea.

2

Harry Kane wa Tottenham akijaribu kupiga shuti mbele ya mabeki wa Chelsea.

3

Nemanja Matic (kulia)  akiwania mpira na Erik Lamela wa Tottenham. 

KLABU za Chelsea na Tottenham leo zimeshindwa kutambiana na kutoka suluhu katika mtanange wao wa Ligi Kuu ya England uliopigwa jioni hii kwenye Uwanja wa White Hart Lane.

Kwa matokeo hayo, Chelsea wanaosuasua katika ligi hiyo wamefikisha pointi 15 wakiwa nafasi ya 14 huku Tottenham wakiwa na pointi 25 katika nafasi ya 5.

Mpaka sasa kinara wa ligi hiyo ni Mancester City wenye pointi 29 wakifuatiwa na Leicester City ambao nao wana pointi 29 wakitofautiana kwa mabao.

Vikosi vilikuwa hivi:
TOTTENHAM XI (4-2-3-1): Lloris; Walker, Alderweireld, Vertonghen, Rose; Mason (Lamela 55), Dier, Dembele, Son (Njie 73); Eriksen; Kane.

CHELSEA XI (4-2-3-1): Begovic; Ivanovic, Zouma, Cahill, Azpilicueta; Fabregas, Matic; Willian (Kennedy 88), Oscar, Pedro (Loftus-Cheek – 91); Hazard.

Comments are closed.