ESTER KIAMA ARUDI KIJIJINI KULIMA
MWIGIZAJI wa filamu za Kibongo, Ester Kiama ameamua kurudi kijijini kwao, Dumila mkoani Morogoro kuangalia kama anaweza akajishughulisha zaidi na kilimo kuliko kupoteza muda mwingi akiwa mjini. Kiama aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, anadhani anapoteza muda mwingi mjini, wakati angeweza kurudi kijijini na akatafuta namna nyingine ya kupambana na maisha.
Alisema kuna vitu vingi amejaribu kufanya ili tu kwenda na maisha yaliyopo hivi sasa, lakini anaona inakuwa vigumu kukamilisha ndoto nyingi alizokuwa nazo kwa sasa hivyo bora ageukie kilimo.
“Kipindi tulichonacho sasa hivi si cha kuchagua nini cha kufanya, ni vyema kujikita kwenye kazi yoyote ambayo unajua inaweza kukuingizia kipato kizuri na kuweza kujimudu kimaisha, maana maisha ya sasa ni magumu mno, yaani hamna kuchagua cha kufanya,” alisema Kiama
STORI: IMELDA MTEMA, DAR
Comments are closed.