The House of Favourite Newspapers

#Exclusive: Happy Samatta Afichua Alivyowekewa Sumu Kwenye Chakula Uturuki -Video

Mbunifu wa mavazi mbalimbali, Happy Suleiman @khadd_77 ambaye alikuwa akifanya kazi yake hiyo nchini Uturuki, amesema kuwa alisaidiwa na Samatta kama ambavyo hata Diamond angekuwa nchini Uturuki angemsaidia.

Happy amefunguka mengi kupitia Global TV na kueleza jinsi alivyopitia msoto nchini Uturuki akiwa hana chochote na jinsi Samatta alivyomsaidia.

Ameeleza kuwa hata hati ya kusafiria (passport) hakuwa nayo zaidi ya kurudi na karatasi pekee huku akiwa na msongo mkali wa mawazo.