The House of Favourite Newspapers

Fahamu Mambo Muhimu Kuhusu VVU/ Ukimwi

0

Symptoms_of_acute_HIV_infection.svgWiki hii tunachambua Virusi vya Ukimwi (VVU) na ugonjwa wenyewe, tutaangalia hatua kwa hatua hadi mgonjwa anaonekana kuwa ana Ukosefu wa Kinga Mwilini (Ukimwi).

Ili mtu ajulikane kuwa ana VVU /Ukimwi, atapitia hatua nne za lazima kama nitakavyoziainisha.
Hatua ya kwanza hujulikana kitaalam kama Primary HIV Infection ambapo mgonjwa hudumu nayo kwa wiki nne baada ya maambukizi. Watu walio katika maambuki katika hatua hii ni asilimia 20 tu ya wenye Maambukizi ya VVU ambao huona dalili za ugonjwa huu.

Mara nyingi walio katika hatua hii madaktari hushindwa kutambua kama mgonjwa amepata Maambukizi ya VVU kutokana na dalili na viashiria vyake, hufanana sana na dalili za magonjwa mengine.

Kutokana na hilo, madaktari huwa makini sana kwani aliyeambukizwa akiwa katika hatua hii, huonesha dalili kama vile kuvimba tezi yaani swollen lymph glands, kuwa na homa kali, kuumwa koo, yaani sore throat, kujihisi mchovu, kujihisi maumivu sehemu mbalimbali mwilini, kutokwa na vipele mwilini (skin rash) na pia kutapika, kuharisha au kuumwa tumbo.

Mgonjwa mwenye dalili hizo kitaalam hutajwa kuwa amepata Acute HIV Infection/Acute HIV Retroviral Infection au Seroconversion Illness. Hatua ya pili ya VVU/ Ukimwi kitaalam huitwa Clinically Asymptomatic Stage na mgonjwa hudumu nayo kwa miaka 10 na wengi wao hawaoneshi dalili yoyote isipokuwa anaweza kuwa na tezi zilizovimba, yaani swollen lymph nodes.

Lakini ukweli ni kwamba, kiwango cha VVU kwenye damu hupungua sana lakini mgonjwa anaweza kuambukiza mtu mwingine yeyote.Hata hivyo, licha ya mgonjwa kutoonesha dalili za maradhi lakini akienda kwenye vipimo vya VVU vitaonesha kwamba ana maambukizi ya ugonjwa huo katika damu yake.

Wagonjwa wa kundi hili hutakiwa kupima kwa kipimo cha wingi wa Virusi Vya Ukimwi, yaani Viral Load Test kwani VVU katika mwili wanapozaliana hujificha kwenye tezi yaani lymph nodes. Kipimo hiki pia husaidia katika kumpangia mgonjwa tiba yake.

Akitoka katika hatua hiyo, huja hatua inayoitwa kitaalam Symptomatic HIV Infection, hapa kinga za kinga ya mwili huzidi kudhoofika kutokana na kuongezeka kwa VVU kwani tezi na tishu zilizoathiriwa na VVU huharibika kutokana na maambukizi kuwa mwilini muda mrefu na virusi hao hubadilikabadilika na kuwa na uwezo zaidi wa kuathiri tishu na sehemu mbalimbali za mwili na hata kuziua seli zinazokinga mwili (Thelper Cell) kutokana na maambukizi hivyo kushindwa kuzalisha seli nyingine mpya.

MATUMIZI YA ARV’s

Wagonjwa wengi wa Ukimwi huanza kutumia dawa za kurefusha maisha (ARV’S) baada ya kufikia hatua hii. Dawa za hizo hushambulia VVU na huanza kutumiwa wakati seli aina ya CD4 (Cluster of Differentiation), zinapopungua na kuwa kiwango cha chini sana.

Itaendelea wiki ijayo.

Leave A Reply