The House of Favourite Newspapers

FAIZA KUFANYA UPASUAJI WA MATITI

0
FAIZA KUFANYA UPASUAJI WA MATITI
Faiza Ally.

MSANII mwenye vituko kutoka tasnia ya Bongo Fleva, Faiza Ally amefunguka kuwa akimaliza kunyonyesha tu mtoto wake wa pili aliyejifungua hivi karibuni lazima afanye upasuaji wa matiti kuwa binti mdogo.

Akizungumza na Ijumaa katika mahojiano maalum Faiza ambaye ana watoto wawili kwa sasa alisema, tangu amejifungua mtoto wa pili ameongeza furaha na kumfanya kujiamini zaidi.

“Unajua kila kitu ni kupanga kwa sababu huyu baba wa mtoto wangu wa pili ni Mmarekani na hatukuwahi kupanga kuishi pamoja zaidi ya kuja labda kwa mara moja kuona mtoto wake basi.

Faiza kufanya upasuaji wa matiti…

“Kwa sasa sina mpango wa kuongeza mwingine tena nikimaliza kunyonyesha nitaenda kufanya operesheni ya matiti kuyarudisha saa sita yaani nirudi msichana kabisa labda,” alisema Faiza.

NA: IMELDA MTEMA| IJUMAA

Breaking News: Bavicha Wahoji… Kwa ni Chadema Pekee Ndio Wanaokamatwa?

Leave A Reply