Flavour atoa kadi maalum za Krismas kwa mashabiki wake
Mwimbaji maarufu wa Nigeria, Mr Flavour.
MWIMBAJI maarufu wa Nigeria, Flavour Na’abalia, ametoa kadi maalum za Krismas kwa mashabiki na wapenzi wake.
Mwimbaji huyo aliyetamba na kibao cha ‘Golibe’ ambaye anasemekana kuwa katika ‘mahaba niue’ na mwimbaji maarufu wa kike wa Nigeria, Chidimma Ekile, ametoa kadi hizo zenye picha yake ambazo zinamwonyesha akiwa na taswira ya kuvutia.
Katika picha hiyo, Flavour anaonyesha mwili wake wa kuvutia, tatuu kibao na akiwa kifua wazi.