The House of Favourite Newspapers

Forbes: Dangote Bilionea Namba 1 Afrika Mwaka 2017, Mo Dewji wa 20… Orodha Yote Ipo Hapa

JARIDA Maarufu ambalo hufanya tafiti na kuchapisha rekodi mbalimbali za watu kwenye tasnia kadha wa kadha duniani, Forbes limemtaja Mfanyabiashara maarufu kutoka nchini Nigeria, Alhaji Aliko Dangote kuwa ndiye tajiri mwenye mkwanja zaidi barani Afrika akikadiriwa kuwa jumla ya $12.2 bilioni.

Kuna mabilionea (wa Dola) 25 mwaka huu barani Afrika, mmoja juu ya 24 waliokuwepo mwaka jana.

Wafanyabiasha kutoka Nigeria Femi Otedola na Abdulsamad Rabiu hawakufanikiwa kuingia kwenye orodha hiyo mwaka huu.

Mo Dewji

Mtanzania Mohammed Dewji bado ndiye bilionea wa umri mdogo zaidi Afrika, utajiri wake ukikadiriwa kuwa $1.09 bilioni.

Isabel dos Santos kutoka Angola na mfanyabiashara wa mafuta Folorunsho Alakija kutoka Nigeria ndiye mabilionea wanawake pekee katika orodha hiyo mwaka huu.

Bw Dangote Dangote, ndiye mwanzilishi na mwenyekiti wa kampuni ya Dangote Cement inayoongoza kwa kuzalisha saruji Afrika. Anamiliki asilimia 90 ya hisa za kampuni hiyo.

Dangote Cement huzalisha tani 44 milioni za saruji kila mwaka na imepanga kuongeza uzalishaji kwa asilimia 33 kufikia 2020.

Dangote pia anamiliki hisa katika kampuni za chumvi, sukari na unga.

Mohammed Dewji ni afisa mkuu mtendaji wa kampuni ya METL iliyoanzishwa na babake miaka ya 1970. Kampuni hiyo huhusika katika biashara ya nguo, unga, vinywaji na mafuta. Kampuni hiyo huendesha shughuli zake katika zaidi ya mataifa sita barani Afrika.

Mabilionea 25 wa Afrika mwaka 2017:

1. Aliko Dangote, Nigeria

Utajiri: $12.2 bilioni

2. Nicky Oppenheimer, Afrika Kusini

Utajiri: $7 bilioni

3. Mike Adenuga, Nigeria

Utajiri: $6.1 bilioni

4. Johann Rupert, Afrika Kusini

Utajiri: $6.3 bilioni

5. Nassef Sawiris, Misri

Utajiri: $6.2 bilioni

6. Christoffel Wiese, Afrika Kusini

Utajiri: $5.9 bilioni

7. Nathan Kirsch, Swaziland

Utajiri: $3.9 bilioni

8. Naguib Sawiris, Misri

Utajiri: $3.8 bilioni

9. Isabel dos Santos, Angola

Utajiri: $3.1 bilioni

10. Issad Rebrab, Algeria

Utajiri: $3 bilioni

11. Mohamed Mansour, Misri

Utajiri: $2.7 bilioni

12. Koos Bekker, Afrika Kusini

Utajiri: $2.1 bilioni

13. Allan Gray, Afrika Kusini

Utajiri: $1.99 bilioni

14. Othman Benjelloun, Morocco

Utajiri: $1.9 bilioni

15. Mohamed Al Fayed, Misri

Utajiri: $1.82 bilioni

16. Patrice Motsepe, Afrika Kusini

Utajiri: $1.81 bilioni

17. Yasseen Mansour, Misri

Utajiri: $1.76 bilioni

18. Folorunsho Alakija, Nigeria

Utajiri: $1.61 bilioni

19. Aziz Akhannouch, Morocco

Utajiri: $1.58 bilioni

20. Mohammed Dewji, Tanzania

Utajiri: $1.4 bilioni

21. Stephen Saad, Afrika Kusini

Utajiri: $1.21 bilioni

22. Youssef Mansour, Misri

Utajiri: $1.15 bilioni

23. Onsi Sawiris, Misri

Utajiri: $1.14 bilioni

24. Anas Sefrioui, Misri

Utajiri: $1.06 bilioni

25. Jannie Mouton, Afrika Kusini

Utajiri: $1 bilioni

Comments are closed.