‘FORBES’: TAYLOR SWIFT ANALIPWA MKWANJA MKUBWA ZAIDI DUNIANI
JARIDA maarufu la Forbes limeripoti kuwa staa wa muziki kutoka Marekani, Taylor Swift, ndiye mwanamuziki anayelipwa pesa nyingi zaidi duniani miongoni mwa walio chini ya umri wa miaka 30 .
Jarida hilo limesema jana (Jumatano) kwamba anaingiza Dola milioni 185 kwa mwaka (Sh. bilioni 425) , akifuatiwa na mwanamitindo Kylie Jenner anayeingiza kiasi cha Dola 170 (Sh. bilioni 390) huku rapa Kanye West akishika namba tatu kwa kuingiza kiasi cha $150 (Sh. bilioni 343).
Mhariri wa Forbes, Zack O’Malley Greenburg amesema kuwa sehemu ya mapato ya Taylor Swift imetokana na maonyesho ya jukwaani.
Comments are closed.