TAMASHA la Full Dozi lililoandaliwa na ITV, Redio One na Capital Redio ambalo lilifanyika usiku wa kuamkia Jumapili ndani ya Ukumbi wa Burudani wa Taifa wa Dar Live, lilikuwa kivutio cha aina yake.
Katika burudani hiyo wasanii mbalimbali waliojumuika, walifanya vitu adimu kwa mashabiki waliojaa ukumbini hapo na kuufanya uonekane mdogo.
Wasanii hao ni Snura Mushi, Nature, Sharo Mwamba, Beka Flavour, Q Chilla, Hamorapa na bendi ya muziki wa dansi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’.
Tamasha hilo limeacha gumzo kutokana na kukidhi haja ya mashabiki hao ambao mara kwa mara ‘waliwavamia’ wasanii kama Juma Nature, Q Chilla, Beka Flevour na kuwatunza huku wakiwaomba kurudia nyimbo zao kila walipomaliza kutumbuiza.
Baada ya kumalizika kwa tamasha hilo mashabiki wengi walitaka burudani kama hiyo ifanyike kila mwaka ili kutoa fursa ya aina hiyo kwa watu wengi zaidi.
Na Issa Mnally/GPL