The House of Favourite Newspapers

Gabriel Jesus wa Man City Anukia Juventus

0

KLABU ya Juventus, imetajwa kuwa imeendelea kukomaa na dili la kutaka kumsajili straika wa Manchester City, Gabriel Jesus.

Imeelezwa kuwa, Juventus ipo tayari kutoa fedha ambazo Man City itahitaji kwa ajili ya kumpata straika huyo raia wa Brazil.

 

Juventus inapambana kusaka straika bora kwa ajili ya msimu ujao ambaye atashirikiana na Cristiano Ronaldo.

 

Jesus amekuwa hana namba ya moja kwa moja katika kikosi cha Man City chini ya Kocha Pep Guardiola hasa kwa msimu wa 2020/21.

 

Hivi karibuni, Guardiola alinukuliwa akisema hana mpango wa kusajili straika mwingine baada ya kuondoka kwa Sergio Kun Aguero, huku akipanga kuwatumia Jesus, Ferran Torres na Riyard Mahrez.

 

Wakati Juventus ikipambana kumsajili Jesus, imeelezwa kwamba ina mpango wa kumrejesha nyota wake, Moise Kean kutoka Everton, ingawa wamesema watafanya hivyo kama kutakuwa na ulazima.

⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP: ⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8 ⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx

Leave A Reply