The House of Favourite Newspapers

Genk Inamlimpa Mbappe Mil 30

MSHAMBULIAJI kinda wa Tanzania, Kelvin John ‘Mbappe’ ameyaanza maisha mapya katika klabu ya KRC Genk huku akilipwa zaidi ya milioni 30 za mshahara kwa mwezi.

Mbappe aliondoka wiki iliyopita kuelekea nchini Ubelgiji kujiunga na timu ya Genk ya vijana, ambapo muda mfupi baada ya kuwasili mabosi wa klabu hiyo wakampeleka kwenye ya Brooke House College and Football Academy, iliyopo kwenye mji wa Leicester kwa ajili ya kupata elimu ya dunia na kisoka ambapo atadumu hapo kwa muda wa miaka miwili.

Akizungumza na Spoti Xtra akiwa nchini Uingereza, Mbappe alisema; “Ingawa kwa sasa sipo Ubelgiji, nipo kwenye moja ya Akademi huku London England, ambapo nitakuwa hapa hadi nitakapofi kisha miaka 18, kuhusu mshahara siyo mbaya ila ni siri yangu.” Lakini uchunguzi wa Spoti Xtra umejiridhisha kwamba atakuwa akikinga zaidi ya Mil 30 kwa mwezi.

Comments are closed.