The House of Favourite Newspapers

Giggs Ashitakiwa Kuwanyanyasa Wanawake

0

MENEJA wa Klabu ya Wales, Ryan Joseph Gigs anashitakiwa makosa matatu ya unyanyasaji dhidi ya wanawake wawili. Anashutumiwa kwa kusababisha madhara ya mwili kwa mwamke aliye na umri wa miaka zaidi ya 30 na unyanyasaji wa kawaida dhidi ya mwanamke mwingine mwenye umri wa zaidi ya miaka 20 katika eneo la Salford, Novemba 2020.

 

Giggs (47), wa Worsley, pia anashitakiwa kwa kosa la kulazimisha au tabia ya kuthibiti. Amepewa dhamana ya kufika katika makakama za hakimu mkazi za Manchester na Salford, Aprili 28. Giggs alisema katika taarifa yake kwamba atakana mashitaka mahakamani.

 

“Ninaheshimu kabisa mchakato wa shetia na ninafahamu ukubwa wa madai,” alisema.

“Ninasubiri kusafisa jina langu.”

 

Polisi wa Manchester Police walisema maafisa wa polisi waliitwa saa nne na dkika tano za usiku tarehe 1 Novemba kutokana na taarifa za usumbufu zilizotokea katika eneo la Worsley.

 

Polisi walisema kuwa mwanamke mwenye miaka zaidi ya 30 alitibiwa majeraha madogo katika eneo la tukio. Giggs pi anashutumiwa kwa tabia ya kulazimisha na mienendo ya kudhibiti anayodaiwa kutekeleza katika miezi ya Disemba, 2017 na Novemba, 2020.

 

Shirikisho la Soka la Wales (FAW) limethibitisha meneja msaidizi Robert Page h atachukua usukani wa timu hiyo kuanzia msimu huu wa Championi Lig.

 

FAW lilisema kutakuwa na mkutano wa bodi ya klabu hiyo “kujadili suala hilo na athari yake kwa shirikisho na timu ya taifa “.

 

Katika taarifa yake, Bw Giggs alioneza kuwa: “Ningependa kumtakia Robert Page, makocha, wachezaji na mashabiki kila mafanikio katika michuano ya Eropa msimu huu.”

 

Winga huyo wa zamani wa Manchester United ni mmoja wa wacheza waliotunukiwa tuzo zaidi nchini Uingereza baada ya miaka 24 ya mchezo wake katika Old Trafford na aliteuliwa kuwa OBE mwaka 2007 kabla ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa BBC mwaka 2009.

 

Pia alishinda kofia 64 za mchazaji bora wa Wales kati ya mwak 1991 na 2007 na aliteuliwa kuwa meneja wa taifa wa Wales Januari,2018, ambapo aliongoza timu ya taifa hilo kufuzu michezo ya Ulaya 2020, ambayo iliahirishwa kwasababu ya Covid-19. Pia ni mmiliki mwenza wa timu ya Ligi ya daraja la pili ya Salford City.

Leave A Reply