Gigy Money Adai Unga, Pombe Vinatesa Mastaa wa Bongo, Agusia na Bangi
GIFT Stanford almaarufu Gigy Money; ni mwanamama staa wa muziki nchini Tanzania ambaye amefichua siri ya mastaa wengi Bongo kuwa wana njaa inayowasababisha kuishia kuteswa na matumizi ya madawa ya kulevya (unga), bangi na pombe.
Gigy anasema kuwa kibaya zaidi hawana elimu ya matibabu ya kuondokana na msongo wa mawazo na kuishia kulalamika wasijue namna ya kujinasua huko.
“Mastaa wengi wa Bongo wanaishi kwenye njaa mpaka unawakuta wamepigwa picha wakiwa wamekondeana kwa sababu ya cocaine (unga), weed (bangi) na alcohol (pombe).
“Na kibaya zaidi Wabongo wengi hawajui kufanya therapy (tiba ya kuathirika na msongo wa mawazo) na ninamshukuru sana marehemu Ruge Mutahaba ndiye aliniambia ninahitaji mtu wa kuniweka vizuri kisaikolojia, therapist; mtu wa matibabu ya akili ni mambo ambayo wanapaswa kujifunza,” anasema Gigy ambaye ni mama wa mtoto mmoja.
Cc; @sifaelpaul