The House of Favourite Newspapers

Gigy Money Amalizana na Mpenzi Wake

MWANADADA ambaye ni mwana-muziki na muuza sura kwenye video za Kibongo, Gift Stanford ‘Gigy Money’, hivi karibuni amefunguka kwamba, hana matatizo tena na baba wa mtoto wake mtarajiwa aitwaye Mo Jay, na kwamba kila kitu kwa sasa wamekwisha kiweka sawa ambacho kilikuwa kinawafanya wagombane mara kwa mara.

 

Akichonga na Showbiz Xtra, Gigy aliongeza kuwa, wawapo wawili ‘tafaruku’ ndogondogo huwa hazikosekani, jambo ambalo lilikuwa linajitokeza kwao, lakini kwa sasa kila kitu kipo sawa na hawana tatizo kabisa.

 

“Sina shida yoyote na mpenzi wangu kwa sasa, kila kitu kipo sawa na yakiwepo ya kuzun-gumza kama tuna matatizo nitazu-ngumza huko mbele, lakini kwa sasa hakuna tatizo lolote,” alisema Gigy.

BONIPHACE NGUMIJE.

MAMA DOGO JANJA ATIA NENO LA VALENTINE KWA UWOYA

Comments are closed.