Mbowe akiongozana na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya Sophia Mwakagenda wamefika mahakamani hapo kwa ajili ya kusikiliza kesi hiyo ambayo inasikilizwa mfululizo kwa wiki hii yote.
Jana jumanne mahakama hiyo ilikataa kutoa dhamana kwa mbunge huyo na kuamuru arudishwe rumande wakati ushahidi wa kesi yake ukianza kusikilizwa kuanzia hii leo.
Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ anakabiliwa na kesi kutoa maneno ya uchochezi dhidi ya Rais wa Jamhuri ya muungano Dkt John Magufuli wakati wa mkutano wake wa hadhara uliofanyika mwishoni mwaka jana. Mwisho.


Comments are closed.