Hoja hizo ilikuwa wasomewe Novemba 15, 2016 lakini zilikwama kusomwa kutokana na Lema kuugua ghafla na Wakili wa Serikali, Elizabeth Swai kumuomba hakimu kutumia busara ya Mahakama kuisogeza mbele kesi hiyo kutokana na hali ya mbunge huyo.
Awali, upande wa Jamhuri ulidai utakuwa na mashahidi watano katika kesi ya kuhamaisha maandamano na upelelezi umekamilika.
Mashahidi wengine ni ASP Damas Masawe ambaye ni (OCCID), Inspekta Adam Nyamiti, WP 6826 DC Esta Yohana na Ezekiel Denis Kwayu kutoka kitengo cha Upelelezi Makao Makuu ya Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam.
Kwa upande wa kesi ya Lema na mkewe ya kumtumia ujumbe wa matusi Gambo, itaanza kusomwa maelezo ya awali ambayo nayo itakuwa tayari kwa kuanza kusikiliza baada ya upelelezi kukamilika.
Comments are closed.