The House of Favourite Newspapers

Gomes Apata Timu Mauritania

0

Aliyekuwa Kocha wa Simba, Didier Gomes Da Rosa, ametangazwa kuwa Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa Ya Mauritania.

 

Gomes ambaye aliachana na Simba, Oktoba mwaka huu, amewahi kufundisha vilabu vya Al-Ismaili, Al-Marreikh ya Sudan, na Simba ya Tanzania.

 

Gomes anakwenda kuchukua nafasi ya Mfaransa mwenzake Corentin Da Silva Martins, ambaye alifungashiwa virago baada ya matokeo mabaya katika mechi za kufuzu kwa Fainali za Kombe la Dunia Qatar 2022.

 

Didier Gomez ataanza kibarua chake na Mauritania katika Mashindano yanayokuja ya Kombe la “Arab Cup” yatakayofanyika Qatar.

Leave A Reply