The House of Favourite Newspapers

Gomes: Azam FC ni Njia ya Kwenda Fainali FA

0

BIG bosi wa Benchi la Ufundi la Simba, Didier Gomes raia wa Ufaransa amebainisha mapema kwamba wapinzani wao, Azam FC ni njia ya wao kutinga Hatua ya Fainali ya Kombe la Shirikisho (FA).

 

Kocha huyo ameongeza kwamba anataka kuiona timu yake ikifanikiwa kutinga fainali ya michuano hiyo kwa ajili ya kutimiza malengo ambayo alijiwekea ambapo hilo haliwezi kutimia bila ya kuwafunga Azam FC.

 

Simba watakutana na Azam FC kwenye nusu fainali ya FA baada ya timu hizo kushinda mechi zao za robo fainali za michuano hiyo.

Gomes raia wa Ufaransa, amebainisha wazi kwamba anataka kuiona Simba ikitinga fainali ya michuano hiyo ambapo haiwezi kufanya hivyo bila ya kuwaondosha Azam FC katika nusu fainali.“Tumefika nusu fainali, hili ndilo lengo letu tangu mwanzo.

 

Niliwaambia wachezaji wangu kwamba tunataka kufika fainali moja mwaka huu na kushinda.“Tuna hatua moja ya kucheza ya nusu fainali, lakini tuko kwenye mwendo mzuri na najivunia sana wachezaji wangu wanavyojitoa. Tunaweza kufikia malengo mawili ambayo tumejiweka msimu huu,” alimaliza Gomes.

STORI NA SAID ALLY | CHAMPIONI

Leave A Reply