The House of Favourite Newspapers

Kero ya Maji Kishapu Shinyanga

Mkazi wa kata ya Mwadui Lohumbo wilayani Kishapu akichota maji ya kunywa baada ya kufukua mchanga pembezoni mwa mto Tungu unaotenganisha wilaya ya Maswa mkoa wa Simiyu na Kishapu mkoa wa Shinyanga,mto huo ni tegemeo kubwa la wananchi wa wilaya ya Kishapu kutokana na uhaba wa maji.

WAKATI nchi yetu Tanzania ikiadhimisha wiki ya maji, imeelezwa kuwa wanawake wengi wilayani Kishapu mkoani Shinyanga wamekuwa wakitumia muda mwingi kutafuta maji hivyo kushindwa kushiriki katika shughuli za maendeleo kikamilifu.

Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea wilayani humo wananchi wa vijiji vya Nyenze na Ng’wang’holo kata ya Mwadui Lohumbo wilayani humo walisema maji ni changamoto kubwa inayorudisha nyuma maendeleo ya wananchi kwani wanatumia muda mwingi kutafuta maji.

Mkazi wa kata ya Mwadui Lohumbo wilayani Kishapu akichota maji ya kunywa baada ya kufukua mchanga pembezoni mwa mto Tungu.

Msemaji huyo alifungukua kuwa licha ya kuishi karibu na mgodi wa almasi wa Williamson bado wanalazimika kutembea umbali takribani kilomita tano kufuata maji katika mto Tungu unaotenganisha wilaya ya Kishapu na wilaya ya Maswa mkoa wa Simiyu.

Mkazi wa kata ya Mwadui Lohumbo wilayani Kishapu akitoka mto Tungu kuchota maji ya kunywa.

Mashimo yaliyofukuliwa pembezoni mwa mto Tungu ambapo maji hujichuja kutoka kwenye mto na kuingia kwenye mashimo hayo na wananchi kuchota maji hayo kwa ajili ya kunywa.
Wananchi wakifua nguo katika mto Tungu.
Wananchi wakifua nguo katika mto Tungu.

Comments are closed.