Haji Manara: Yanga ni Klabu Kubwa, Itashinda Kila Taji – Video
“Siendi Yanga kwa sababu ya jambo lolote, ninaamini Yanga watanipa nafasi ambayo nitaitumikia, kule nilibanwa sana, sina tatizo na Simba, nilisema vizuri kabisa kwamba sijawahi kuwa na tatizo na Simba, walionifanyia nimeshayasema.
“Ninachoomba viongozi mnipe sapoti tuijenge Yanga, kama mliniona Simba nikiwa vile, huku nitakuwa mara kumi. Shukrani yangu kwenu ni kufanya kazi kwa asilimia 100, niwahakikishie baada ya Desemba, Yanga itakuwa kila kitu. Mimi ndio nilikuwa nawabeba, sasa hivi wanahangaika tu, hata jambo lao wameshindwa wala sitawacharura.
“Mimi nina moyo, ofa ya Yanga angekuwa mtu mwingine angesaini hapo hapo, nimeshauriana na familia yangu, nawashukuru Simba kwa sapoti yenu sasa ni zamu ya kuifanyia kazi Yanga. Mabingwa mara 27.
“Yanga ni kubwa mno, sio timu ya kulalamikia TFF wala Bodi ya Ligi, twendeni tukafanye kazi, tutashinda uwanjani, tutengeneze confidence kwa viongozi, wachezaji na mashabiki wetu. Nitafanya kazi kama punda mwenye njaa kuhakikisha Yanga inatimiza malengo yake.
“Mtauliza kwamba nilikuwa nawacharura Yanga, hiyo ndiyo soka, niliwatumikia Simba lakini sasa hivi ni zamu ya Yanga, ndio maana nimevaa jezi ya Yanga, mama Yangu na mke wangu wapo hapa. Tamasha la Jumapili njooni uwanjani, nawaambia haijawahi kutokea.
“Naongea kama msemaji wa Mabingwa mara 27, kesho saa 5:00 tunakwenda kuzindua jezi kweli, haina makorokoro, jezi ya mpira, jezi ya nyumbani, ya ugenini na kit ya tatu na casual wear pale Mlimani City,” amesema Haji Manara, Msemaji wa Yanga.