The House of Favourite Newspapers

Hali Tete… Vigogo Man United Wamjadili Ole

0
MKURUGENZI Mtendaji wa Klabu ya Manchester, Richard Arnold amevunja appointment zote za vikao ili kukutana na Mmiliki wa Klabu hiyo, Joel Glazer kwa ajili ya kujadili hatima ya Kocha wa Klabu hiyo, Ole Gunnar Solskjaer baada ya kipigo ha jana cha bao 5-0 nyumbani dhidi ya Liverpool.
 
Man United imekuwa haina matokeo mazuri kwa mechi za hivi karibuni licha ya usajili mkubwa walioufanya wa Cristiano Ronaldo.
 
Wengi wanasema, Ole aondoke Man U kwani timu ni kubwa kuliko uwezo wake na kwamba kocha huyo ameishiwa mbinu za kuwafundisha mashetani hao wekundu.
Leave A Reply