Hamorapa Anaswa Akinunua Kanzu Ya Idd
Harmorapa ambaye ni msanii wa Bongo Fleva, amebambwa katika soko la Kariakoo jijini Dar kwenye duka moja maarufu la kuuza kanzu linaloitwa Kanzu Empire, akijinunulia kanzu kwa ajili ya Sikukuu ya Idd inayotarajiwa kuwa Jumapili au Jumataju ijayo.
Akizungumza na mtandao wa Global Publishers, Hamorapa sliyeongozana na bosi wake, Irene Sabuka alisema ameona ajipongeze kwa kujinunulia kanzu nzuri baada ya kufanikiwa kufunga mwezi mzima wa Ramadhan bila kupumzika. Jina lake halisi msanii huyu asiyeishiwa kiki ni Athuman Omary.
“ Yaani nimekuja dukani hapa kujipongeza kwa kujinunulia kanzu nzuri kwa sababu niliweza kufunga mwezi mzima hivyo nikaona natakiwa kwenda msikitini nikiwa nimependeza” alisema Hamorapa.