Harmo Rapa Kuachia Kichupa Kipya Soon, Yapo Pia Ya Kufahamu Kuhusu Ile Gari Na Zile Pesa – (Tweets)
Leo kwenye exclusive interview za Global TV Online, tulitembelewa na Harmo Rapa msanii chipukizi anaekuja kwa upepo mkali sana.
Kwenye interview yake, Harmo Rapa aliongelea na kufafanua baadhi ya tetesi zilizokuwa zinasambaa kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo ukweli juu ya gari alilolipost kwenye Instagram, video queen aliyesemekana ni mpenzi wake alafu akakamtosa na mengineyo.
Kikubwa na cha kwanza kabisa kufahamu ni kwamba Harmo Rapa yupo njiani kuachia kichupa kipya…
#Exclusive: Tupo na Harmo Rappa studioni, tutegemee video mpya kutoka kwake very soon!
— Global Publishers (@GlobalHabari) February 17, 2017
Hapa chini nimekusogezea tweets zote tulizokuwa tunafanya wakati wa interview ya Harmo Rapa, karibu uzipitie kisha kumbuka kwenda kusubscribe kwenye YouTube channel yetu ili uweze kuitazama full interview ya Harmo Rapa pale itakapo ruka hewani.
Exclusive live tweets zilikuwa kama hivi:
Kuhusu zile pesa alizoonekana akizihesabu Instagram:
#Exclusive: “Zile pesa nilizopiga nazo picha ni hela tu ya biashara yetu, ninafanya biashara na bossi wangu.” – Harmmo Rappa.
— Global Publishers (@GlobalHabari) February 17, 2017
Na ile gari je?
#Exclusive: “Kuhusu ile ndinga, ndio ile ni ya kwangu. Ni zawadi niliyozawadiwa na bossi wangu… ” – #HarmmoRappa.
— Global Publishers (@GlobalHabari) February 17, 2017
#Exclusive: “Kwa sasa naendeshwa na bossi wangu kwasababu bado sina leseni. Ila nafanya mpango, nitaipata hivi karibuni.” –#HarmmoRappa
— Global Publishers (@GlobalHabari) February 17, 2017
Tunasikia kuwa yule video queen kwenye wimbo wak wa kwanza alikuwa mtu wako na badaae akakutosa… ni kweli?
#Exclusive: “kuhusu yule video queen, yule sio mtu wangu. Yule alikuwa ni video queen tu biashara yetu iliishia pale” – #HarmmoRapa
— Global Publishers (@GlobalHabari) February 17, 2017
Ujumbe kwa watu wasioamini kuwa unaweza kufanya muziki:
#Exclusive: “Wale wanaonikataa leo, IPO Siku watanikubali… Ipo siku watanikubali tu!” – #HarmmoRapa
— Global Publishers (@GlobalHabari) February 17, 2017
Usisahau kusubscribe kwenye YouTube channel yetu ili uweze kuitazama full interview ya Harmo Rapa pale itakapo ruka hewani.
Comments are closed.