Harmonize Afunika Mlimani City (Picha +Video)
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Abdul Kahali maarufu Harmonize au Konde Boy usiku wa kuamkia leo alijaza umati mkubwa wa mashabiki ndani ya Ukumbi wa Mlimani City, Dar wakati akizindua albamu yake ya Afro East.
Katika shoo hiyo pamoja na kufurika wageni waalikwa zaidi ya 500 pia ilivamiwa na mashabiki zake wengine zaidi ya idadi hiyo na kupafanya eneo hilo litapike watu na kukosekana pakukanyaga.
Kutokana na kufurika kwa umati eneo hilo nusu ya mashabiki waliofika eneo hilo waliishia nje kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kukosa kadi mwaliko au waliotaka kutumia kadi moja kwa zaidi ya mtu mmoja.