The House of Favourite Newspapers

Harmonize Amuandikia Ujumbe Mzito Mavoko

0

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Harmonize leo Mei 6, 2020 ametumia ukurasa wake wa Instagram kuandika ujumbe mzito sana unaomhusu Rich Mavoko ambaye walifanya kazi wote WCB ingawa kwa sasa wote hawapo Wasafi.

Harmonize ameandika:

Familia Ngapi Zipo Nyuma Ya @richmavoko ..?? Na zinamtegemea Yeye KwaKila Jambo Hasa Hili La Kupata Mkate Wa Kilasiku VP Kuhusu Ndoto Za Familia Hizo Na Zinaishije Katikwa Wakati Huu…???
Ndoto Ngapi Za Wasani Ambao Wanategemea Kuzifikia Hizo Ndoto Kupitia Mavoco ..?? Na Nyuma Ya Hao Wasanii Kuna Familia NyenginePia ..??

Jeee Maumivu Malala Miko Ya Wazazi Wake Hasa Mama Mzazi Ambae Ndio Kama Roho Yake …!!! Ushajiuliza Ni Kauli Ngapi Za Uchungu Anazitoa Ambazo Zinaweza Kumpata Kila Anaefurahishwa Na Hili Kwa Makusudi ..???

Mana Mzazi wa Mwenzio Ni wako Pia Laana Yake Haishindwi Kukupata …!! La Mwisho Kabisa Mgeukie Mwenzio Anaefurahia Na Kuifanya Hii Kuwa Ni Habari Njema Kwake Ya Kumfanya Atembee Kifua Mbele Na Hata Kuandika Mtandaoni Kwa Furaha MAVOCO KAPOTEA muulize Anafaidika Nanini …???

Mungu Anasababu Na Maana Yake Bro @richimavoco Kama Mdogoako Nakuombea Najua Ukimya Wako Unamaana Kubwa Sanaa Ndani Yako Ninachojua Ni Kujiweka Sawa Na Kutuletea Kazi Zingine Tunakupenda Na Tunakuombea Mungu Akufanyie Wepesi…!!! Let’s Go Bro Mdogoako Rafiki Yako Nipo Hapa Muda Wowote…!!!! RAMADAN KAREEM”

Huo ndio ujumbe wa Harmonize kwa Mavoko.

Leave A Reply