The House of Favourite Newspapers

Harmonize: Mama Dangote Alikuwa Ananichora Tu!

0


MWANAMUZIKI Harmonize leo Novemba 18, 2021 amemfungukia mama mzazi wa msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, Sanura Kassim, maarufu mama Dangote, baada ya kwenda kumueleza nia yake ya kuondoka  katika
Lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB) iliyo chini ya Diamond Platnumz.

Kauli za Harmonize;-

“Kumbe nilivyoenda kwa mama Dangote kumuelezea, alikuwa ananichora tu huku, moyoni ameshaweka ‘unataka kumpita mwanangu’.

“Hadi kwenye lebo ikawa inaonekana natengwa. Nikamfuata na kumuuliza (Diamond) bro niambie kuna tatizo gani, akawa haniambii, kila siku maneno mapya.

“Mara naambiwa nimeenda Nigeria nimefanya kolabo na msanii wa Nigeria kisha unanikata dola 5,000, hiyo hela ukii-change inakuwa Sh milioni 12. Mimi ni mtoto wa masikini, hiyo hela ningeweza kuwasaidia watu wengi walio nyuma yangu.

“Burna Boy akaenda Rwanda, kanipigia simu niende nika-perform, nilikuwa kwenye lebo nikacheki na management nikawaeleza.

“Wakaniambia nikitaka kwenda natakiwa nitoe dola 10,000. Nikasema haina noma, nikaenda ila siku-perform.

“Kumbe wao kwenye shoo walipanga wimbo wa Kainama uwe wa mwisho kwenye playlist yao, imefika muda unapigwa sionekani jukwaani, walisikitika sana,” amesema Harmonize baada ya kutua Dar es Salaam, leo Alhamisi akitokea Marekani.

HARMONIZE ALIVYOTUA BONGO, AVUJISHA SAUTI YA RAYVANNY, AMLIPUA DIAMOND VIBAYA, AANIKA UKWELI

Leave A Reply