The House of Favourite Newspapers
gunners X

Hassan Mwakinyo Amchapa Eribo kwa KO Raundi ya Pili

0

Bondia nyota wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameendeleza ubabe baada ya kushinda kwa knockout (KO) dhidi ya mpinzani wake kutoka Nigeria, Eribo, katika pambano lililofanyika usiku wa leo kwenye Ukumbi wa Warehouse, Masaki — Dar es Salaam.

Mwakinyo alimaliza kazi ndani ya mizunguko miwili tu, akitumia umakini na kasi kubwa, jambo lililowafanya mashabiki waliokuwa ukumbini kusimama kwa shangwe.

Ushindi huo umeonekana kama faraja kwa Watanzania wengi, hususani baada ya timu ya taifa, Taifa Stars, kupata matokeo mabaya dhidi ya Nigeria kwenye michuano ya AFCON 2025.

Mwakinyo ameahidi kuendelea kupambana na kuipa heshima Tanzania kimataifa kupitia ndondi.

BAADA ya CATHERINE KUMLILIA KAKA YAKE kwa UCHUNGU HATIMAYE AMEACHIWA HURU na MAISHA YAMEANZA UPYAAA!

Leave A Reply