The House of Favourite Newspapers

Hatimaye Chama Arejea Simba

0

KLABU  ya Simba leo Januari 14, 2022 imethibitisha  kukamilisha usajili wa kwa kiungo mshambuaji  wa Zambia Clatous Chota Chama.

Chama amejiunga na Simba akitokea Rs Berkane ya Morocco kwa mkataba wa miaka miwili alijiunga na Simba mwaka 2018 na kuondoka mwaka 2021 kabla ya kurejea Simba na kutambulishwa rasmi leo ambapo bango kubwa lililotolewa na Simba likiwa na picha ya Chama linasomeka “Karibu nyumbani, Welcome home”

Chama aliondoka Simba Augusti 13,  2021 na kujiunga  na RS Berkane ya Morocco na sasa anarejea baada ya kudaiwa kushindwa kuzoea mazingira nchini Morocco.

Leave A Reply