The House of Favourite Newspapers

HUDEFO Ilivyoazimisha Siku Ya Dunia Kwa Kusafisha Mazingira Ufukweni

Dar es Salaam 22 Aprili 2023: Shirika lisilo la kiserikali la Human Dignity and Enviromental Care Foundation (HUDEFO) leo limeazimisha Siku ya Dunia kwa kusafisha mazingira pembezoni mwa Ufukwe wa Mikoko Beach Msasani jijini Dar.

Katika zoezi siku hii ambayo huazimishwa duniani kote HUDEFO wameungana na wadau mbalimbali kusafisha mazingira hayo ambayo yamekuwa hatarishi kutokana na mrundikano wa taka zinazohatarisha usalama wa viumbe hai waishio majini na nchi kavu.

Katika zoezi hilo HUDEFO wameungana na taasisi ya nyingine pamoja na wanafunzi wa Sekondari ya Agape ya Mbagala jijini Dar ambapo kwa pamoja walifanikisha zoezi hilo.

Kwa mawasilino zaidi kuhusu shughuli za hudefo wasiliana nao kupitia 

EMAIL

[email protected]

PHONE NUMBER

+255 786 625 969 +255 759 767 602

LOCATION

Ada estate-Kinondoni District opposite Dar Free Market Mall. P.O.Box 80726 Dar Es salaam, Tanzania.