TOVUTI ya Global Publishers ambayo ni namba moja hapa nchini kwa habari za burudani, michezo, kitaifa, kimataifa, siasa, breaking news na hadithi za kusisimua imempata mshindi wa shindano la kubashiri matokeo ya mchezo wa Fainali ya Kombe la Mapinduzi kati ya Azam FC na Simba SC uliopigwa usiku wa jana Januari 13, 2017 kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Katika mchezo huo Azam ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na dakika ya 13 na kiungo Himid Mao ‘Ninja’ ambalo lilidumu mpaka mwisho wa mchezo.
Mshindi ambaye amefanikiwa kubashiri kwa usahihi matokeo ya mchezo huo ni Abubakar Chibu Jr kutoka Mwananyamala jijini Dar es Salaam ambaye alikuwa ni wa kwanza katika watu walio-comment kwenye ukurasa wetu wa Facebook kubashiri matokeo ya mchezo huo.
Namba yake ya simu ni 0657082300.
Endelea kutembelea tovuti yetu kwa stori moto moto na bahati nasibu za kumwaga.
Comments are closed.