Ibaada ya Kumuombea Rais Magufuli yafanyika London, Uingereza
Picha maalumu ya rais Magufuli (chini) ni sehemu ya wanakwaya.
Askofu mkuu wa kanisa la CCBC, Dk. Sarpong kutoka Ghana na Pastor Bob kutoka Kenya wakiongoza Ibada hiyo.
Mgeni rasmi Naibu Balozi , Msafiri Marwa akitoa neno la Shukurani kwa waandaaji na wahudhuriaji.Baadhi ya Watanzania, wahamasishaji wakiwa na bendela ya Tanzania.Sehemu ya wahudhuriaji.
HAPA KAZI TU! Waafrika waishio jijini London, Uingereza, Desemba, 28 mwaka huu walifanya maombi maalumu ya kumuombea Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli.
Dhumuni la maombi hayo ni kukubali kasi na utendaji wa rais Magufuli pamoja na kuiombea Afrika nzima kupata viongozi wenye hulka kama yake.
Maombi hayo yaliyoandaliwa na Wachungaji wa Kanisa la Calvary Charismatic Baptist Swahili Service jijini huo yalifanyika katika kanisa hilo lililopo 119 East India, Dock Road Poplar London EI46DE, huku mgeni rasmi akiwa ni Naibu Balozi wa Tanzania nchini humo, Msafiri Marwa.
Na Gabriel Ng’osha- GPL