IBADA ya kuuaga mwili wa dada wa Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Global Group, Eric Shigongo, marehemu Vaileth James Bukumbi, imefanyika leo Ijumaa, Juni 21, 2019, nyumbani kwao katika Kijiji cha Bupandwamhela, Buchosa – Sengerema mkoani Mwanza.
Mwili wa Vaileth ambao uliwasili nyumbani kwao jana Alhamisi kutokea nyumbani kwake, Nyamhongolo jijini Mwanza, utazikwa leo kijijini hapo katika eneo la makaburi ya familia.
Viongozi mbalimbali wa serikali, dini, vyama, taasisi na mashirika mbalimbali wamefika nyumbani hapo kwa ajili ya kuungana na waombolezaji kuuaga na kuusindikiza mwili wa mpendwa wao huyo katika nyumba yake ya milele.
PICHA NA DENIS MTIMA NA IDD MUMBA | GPL
Comments are closed.