The House of Favourite Newspapers

Ihefu Yaendelea Kuiwinda Yanga

0

IKIWA Ligi Kuu Bara inatarajiwa kuendelea Julai 14, mwaka huu baada ya mechi za viporo kumalizika, Ihefu FC inaendelea kujifua ikiiwinda Yanga.

 

Timu hiyo ngeni ndani ya Ligi Kuu Bara ikiwa na maskani yake Mbarali mkoani Mbeya, Julai 14, mwaka huu itacheza dhidi ya Yanga kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar.

 

Akizungumza na Spoti Xtra, Ofisa Habari wa Ihefu, Peter Andrew, alisema wanaendelea kujipanga kuhakikisha wanafanya vizuri kwenye mchezo huo sambamba na wa mwisho dhidi ya KMC.

 

“Maandalizi yapo vizuri, tunaendelea kuwawinda wapinzani wetu, siku yoyote kuanzia sasa tunatarajia kuwasilia Dar kwa ajili ya mchezo huo na wa mwisho ambao pia tutacheza huko dhidi ya KMC,” alisema Andrew.

 

Ihefu haipo kwenye nafasi nzuri katika msimamo wa Ligi Kuu Bara ikiwa imekusanya pointi 35 baada ya kucheza mechi 32.Baada ya Julai 14 kucheza dhidi ya Yanga, siku nne mbele itapambana na KMC. Mechi zote zitachezwa Dar.

SIMON MSINJE, Dar es Salaam

Leave A Reply