The House of Favourite Newspapers

ILO Yatunukiwa Tuzo Kwenye Maadhimisho Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi Duniani

0
Mwakilishi wa shilika la kazi duniani nchini (ILO), Getrude Sima akionyesha tuzo waliyotunukiwa na OSHA kwenye maadhimisho ya siku ya usalama na afya mahala pa kazi duniani yaliyofanyika mkoani Morogoro mwishoni mwa wiki. ILO ilitunukiwa tuzo hiyo kwa kuwa taasisi iliyomstari wa mbele katika kubadilishana taarifa za masuala ya usalama na afya nchini, kikanda na kimataifa.
Mwakilishi wa shilika la kazi duniani nchini (ILO), Getrude Sima akihutubia kwa maadhimisho ya siku ya usalama na afya mahala pa kazi duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Morogoro mwishoni mwa wiki, ambapo mwakililishi huyo amebainisha sheria ambazo nchi wanachama wa shirika la kazi duniani inabidi kuzitekeleza ili kuweka mazingira salama kwa wafanyakazi.
Mwakilishi wa shilika la kazi duniani nchini (ILO), Getrude Sima amepokea tuzo waliyotunukiwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) kwenye maadhimisho ya siku ya usalama na afya mahala pa kazi duniani yaliyofanyika mkoani Morogoro. ILO ilitunukiwa tuzo hiyo kwa kuwa taasisi iliyomstari wa mbele katika kubadilishana taarifa za masuala ya usalama na afya nchini, kikanda na kimataifa.
Leave A Reply