The House of Favourite Newspapers

Instagram Yafanya Maboresho Mapya

0

MTANDAO maarufu wa Instagram umefanya maboresho mapya ambapo watumiaji wa mtandao huo ambapo kwa sawa watakuwa na uwezo wa ku-post, ku-upload video na picha katika akaunti zao za Instagram kwa kupitia tovuti/website ya Instagram.

Maboresho haya yatakuwa msaada mkubwa kwa watu wengi sana hasa kwa wanaosimamia akaunti za watu ambao wanatumia kompyuta katika shughuli mbalimbali na kupunguza matumizi ya simu, feature hii imeanza kutumika wiki hii kwa baadhi ya watumiaji na itaendelea kutoka taratibu kwa watumiaji wengine.

Kwa sasa feature ya kupost video zinazozidi sekunde 60 (zaidi ya dakika moja) inayofahamika kama IGTV imeondolewa na badala yake mtumiaji ata-upload video ndefu na fupi kwenye feature moja ya VIDEOS.

Leave A Reply