The House of Favourite Newspapers

Irene Paul awavaa mastaa wanaogombana!

0

Staa wa sinema za Kibongo, Irene Paul.

Imelda Mtema

Mshangao! Staa wa sinema za Kibongo, Irene Paul amewavaa baadhi ya mastaa wenzake wanaolumbana na kutenganishwa na siasa bila kujua kuna maisha baada ya uchaguzi wa Oktoba 25.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Irene alisema kuwa haoni kama ni vyema wasanii kugawanyika na kutengana kimakundi kwa sababu ya siasa ambalo ni jambo la mpito ambapo baadaye kila mtu atarudi kwenye maisha yake ya kila siku.

“Nawaomba wasanii wasijisahau kabisa kuwa maisha yao ya kila siku yatarudi hivyo wajiepushe na kutengeneza mabifu ambayo hayana msingi,” alisema Irene.

JIUNGE NA GLOBAL BREAKING NEWS!

Leave A Reply