Tanzania Solutions Kutoa Tuzo za Tanzania Elimu Awards Agosti 30
WANAFUNZI waliofanya vizuri katika mitihani mbalimbali ya taifa watatunukiwa tuzo siku ya Agosti 31, mwaka huu katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Hafla hiyo ambapo mgeni rasmi atakuwa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Suleiman Jaffo, itaanza saa 9:00 alasiri.
Tuzo hizo ziitwazo Tanzania Elimu Awards, zitatolewa na Kampuni ya Solutions Tanzania Limited, ambayo imeamua kuonyesha kwa vitendo uungaji wake mkono katika kuithamini sekta ya elimu na vipaji vyake.
Lengo la hatua hiyo ni kuongeza hamasa kwa wanafunzi katika masomo yao.
Comments are closed.