Jafo Ataka Soko la Mabibo Lijenge Miundombinu Bora
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Suleiman Jafo, ametembelea soko la ndizi la Mabibo jijini Dar es Salaam ambapo ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Ubungo kujenga miundombinu rafiki ya maji-taka katika soko hilo ili kuliweka katika mazingira salama.
Jafo amesema hakufurahishwa na miundo mbinu ya soko hilo kwani kumejaa tope na uchafu na kusababisha mifereji kuziba. Waziri huyo pia alisema kwamba mapato ya Sh. milioni 90 yanayokusanywa kwa mwezi hayaridhishi, hivyo aliwataka wabuni mipango ya kuweza kuyaongeza mapato hayo.
NA DENIS MTIMA/GPL
Comments are closed.