KAIMU Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Khamis Juma mapema leo amewaongoza waombolezaji kutoa heshima zao za mwisho kwa aliyekuwa Jaji wa Mahakama kuu ya Tanzania, Upendo Msuya aliyefariki dunia hivi karibuni.
Prof. Ibrahim amewaongoza baadhi ya majaji na viongozi wa kiserikali waliofika nyumbani kwake, Tegeta jijini Dar ambapo pia baadhi ya waombolezaji wamepata fursa ya kutoa heshima zao kanisani ilikofanyika ibada fupi ya kumwombea marehemu.
Baadhi ya viongozi wa kiserikali walionekana kutoa heshima zao za mwisho nyumbani hapo ni pamoja na Spika Msaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Anne Makinda, Mbunge wa Kibamba, John Mnyika na wengine wengi
PICHA NA DENIS MTIMA | GLOBA PUBLISHERS