Jaji Siyani Ajitoa Kesi ya Mbowe
Jaji Mustapha Siyani aliyekuwa akiendesha kesi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake amejitoka kuendesha kesi hiyo leo Jumatano, Oktoba 20, 2021, kwa kile alichodai kuwa kwa sababu ya uwingi wa majukumu unaotokana na uteuzi alioupata hivi karibuni.
Jaji Siyani ambaye hivi karibuni aliteuliwa na Rais Samia Suluhu na kuapishwa kuwa Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ametangaza uamuzi huo muda mfupi baada ya kutoa maamuzi ya kesi ndogo ndani ya kesi kubwa ya Mbowe na kutupilia mbali mapingamizi ya Mbowe.