The House of Favourite Newspapers

JB abainisha kinachoiua sanaa!

JBMkongwe wa filamu Bongo, Jacob Stephen ‘JB’.

MKONGWE wa filamu Bongo, Jacob Stephen ‘JB’ ameweka wazi kinachochangia sanaa ya filamu ionekane kama imepwaya na kukosa thamani katika soko kuwa ni wasanii kuishiwa ubunifu na mipango mikakati ya kuendana na mabadiliko ya teknolojia.

Akichonga na kona ya Bongo Movies, JB alisema kuwa sanaa kama sanaa ipo na kamwe haiwezi kufa, isipokuwa vizazi ndani ya sanaa ndiyo hubadilika kulingana na nyakati, lakini mtu yeyote anaweza kuja na kitu kipya kinachogusa maisha ya kawaida na kuwika, kuliko hata waigizaji wakongwe.

“Kwani muziki wa Kongo si ulionekana kama umekufa, lakini baada ya Koffi Olomide kuachia Ngoma ya Selfie, muziki wao haujarejesha heshima yake? Kwa hiyo sanaa huwa haifi ila watu ndiyo huishiwa.

Comments are closed.