Jb atamba ‘kumfufua’ kuambiana
Staa kwenye sinema za Kibongo, Jacob Steven ‘JB’.
Imelda Mtema
Makubwa! Staa bonge la bwana kwenye sinema za Kibongo, Jacob Steven ‘JB’ ametamba kuwa ‘atamfufua’ aliyekuwa mwongozaji mahiri wa filamu katika tasnia hiyo, Adam Kuambiana.
Aliyekuwa mwongozaji mahiri wa filamu nchini, marehemu Adam Kuambiana.
Jamaa huyo ameliambia Amani kuwa, japokuwa Kuambiana ametangulia mbele ya haki lakini atafanya kama bado uwepo wake upo kwa kuwa filamu ambayo ndiyo ilikuwa ya mwisho kuicheza katika kampuni yake ya Jerusalem Films.
“Nahisi Kuambiana ‘amefufuka’ upya. Hii filamu aliyocheza ya Mahabusu ni bonge la sinema na hata ukiiangalia ni kama bado yupo,” alisema Jb