The House of Favourite Newspapers

Je, Umeinyaka Hii Huduma Mpya Kutoka WhatsApp?

0

mg_whatsapp_code_comp

BAADHI ya watumiaji wa Whatsapp wameingiwa na hofu leo baada ya kukuta ujumbe kwenye simu zao wenye maneno ya njano yakielezea huduma itakayokuwa ikitumika kulinda mawasiliano ya App hiyo baina ya mtumaji na mpokeaji wa ujumbe.

Huduma hiyo kwa kitaalam wanaita ‘end-to-end encryption’ ambapo voice calling, chating za group kwenye simu zote za iOS na Android zitakuwa na uwezo wa kutumia huduma hiyo.

UJUMBE WENYEWE HUU HAPA

messages

Hii inamaanisha serikali ama mtu yeyote itakuwa vigumu kusoma meseji zako labda umpatie simu yako na password. Kwa Ujumla hata WhatsApp wenyewe hawatakuwa na uwezo wa kuzisoma meseji za mtu. Ni mtumaji na mpokeaji wa meseji tu ndiyo watakuwa na uwezo wa kuona mejesi waliotumiana wala sio mtu mwingine katikakati.

WhatsApp wamesema, ‘Kuanzia sasa kama wewe na watumiaji wengine wa WhatsApp uliosevu namba zao watatumia toleo jipya la App hiyo (latest version), kila simu utakayopiga/pigiwa, meseji, chating za grupu, picha, video, faili na ujumbe wa sauti utakaotuma utakuwa umelindwa (secured) moja kwa moja kwa njia ya end-to-end encrypted.

‘Wazo ni jepesi tu hapa: ukituma ujumbe, mwenye uwezo ya kuona ujumbe huo ni yule uliyemtumia pekee, au grupu ambalo umetuma ujumbe wako. Hakuna mtu atauona ujumbe huo, sio wahalifu wa mitandao (cybercriminals), hackers wala serikali.

Leave A Reply